Jumatatu 17 Agosti 2026 - 09:00
Hakuna Maendeleo Yatakayopatikana Katika Mchakato wa Israel Kujiondoa

Hawza/ Muungano wa “Wanazuoni wa Kiislamu” wa Lebanon umesema: Katika hali ya kuendelea  mfululizo wa mashambulizi ya adui wa Kizayuni kupitia mashambulizi ya mizinga na ya anga dhidi ya Lebanon, viongozi wa Lebanon hawana uwezo wa kuchukua hatua yoyote ya vitendo ya kukabiliana na mashambulizi hayo.

Kwa mujibu wa Idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, Baraza la Utendaji la Muungano wa “Wanazuoni wa Kiislamu” wa Lebanon katika kikao chake cha kawaida lilijadili maendeleo mapya nchini Lebanon na katika eneo hilo. Katika taarifa iliyotolewa, ilieleza: Katika hali ya kuendelea mfululizo wa mashambulizi ya adui wa Kizayuni kupitia mashambulizi ya mizinga na ya anga dhidi ya miji na maeneo kadhaa ya kusini, na wakati huohuo katika mazingira ya kuendelea kukiukwa kwa mamlaka ya Lebanon, viongozi wa Lebanon hawana uwezo wa kuchukua hatua yoyote ya vitendo ya kukabiliana na mashambulizi haya na wamechagua ukimya kamili mbele ya mashambulizi hayo; bali hata Waziri wa Mambo ya Nje, ambaye anajaribu kuiomba Iran ifungue Mlango wa Hormuz, hajachukua hatua yoyote ya kulalamikia ramani iliyochapishwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Kizayuni, ambayo inaonesha sehemu za kusini mwa Lebanon kuwa ni mali ya utawala huu.

Muungano huu unaamini kwamba: Kushindwa huku mbele ya matakwa ya Marekani na Wazayuni na kujisalimisha kwake, hakuwezi kupelekea kupatikana kwa mamlaka; bali tangu makubaliano ya “Mfumo” na kuhalalishwa kwa kuufanya Muqawama kuwa uhalifu hadi leo, kwa uhalisia, ni udhihirisho wa utumwa na kujisalimisha. Njia ya mazungumzo kati ya Lebanon na Wazayuni haitaleta maendeleo yoyote katika mchakato wa kuondoka katika ardhi za Lebanon zinazokaliwa kwa mabavu; hususan kwa kuzingatia kauli za wazi za Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa adui wa Kizayuni, na Yisrael Katz, Waziri wake wa Vita, kwamba wataendelea kubaki katika ardhi hizo zinazokaliwa kwa mabavu.

Taarifa hiyo iliendelea kusema: Kila mmoja anauliza: Kwa nini viongozi wa Lebanon wanasisitiza kuendelea na mchakato wa mazungumzo?! Na kwa nini hawajiondoi katika mazungumzo haya ili kuchora mkakati mpya, ambao kimsingi ni ule ule mkakati wa zamani ambao hadi sasa umeilinda Lebanon na kuikomboa tena mara kadhaa; mkakati ambao unafupishwa katika “Utatu wa Lazima: Jeshi, Taifa na Muqawama.”

Muungano wa Wanazuoni wa Kiislamu uliwataka viongozi wa Lebanon kujiondoa katika mazungumzo ya moja kwa moja na adui wa Kizayuni na kurejea katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja; mazungumzo ambayo yaanze tu baada ya kutangazwa kwa ratiba maalumu ya kujiondoa kutoka katika ardhi za Lebanon zinazokaliwa kwa mabavu, kusitishwa kwa mashambulizi na kurejeshwa mateka.

Aidha, Muungano wa Wanazuoni ulilaani hatua iliyochukuliwa katika Bunge la Lebanon, ambayo ni ukiukaji wa wazi wa uhuru wa vyombo vya habari kupitia sheria ya habari inayoruhusu mamlaka ya kisiasa kuwakamata waandishi wa habari, na kusema: Jambo hili linatuingiza katika nchi mpya ambayo ndani yake vyombo vya habari huru, ambavyo vinaweza kukosoa utendaji wa mamlaka ya kisiasa, vitakumbwa na mateso mengi. Tunaliomba Bunge lifikirie upya sheria hii na lisiruhusu kuundwa kwa vyama vipya vya waandishi wa habari; vyama ambavyo kwa kuzingatia hali halisi ya Lebanon vitakuwa vyama vya kisiasa na kimadhehebu, na vitadhuru maslahi ya nchi.

Muungano huu pia ulielezea kuchukizwa kwake na hatua ya Waziri Mkuu ya “kumzuia Michel Menassa, Waziri wa Ulinzi, kutoa hotuba ya kueleza mtazamo wa jeshi kuhusu sheria ya msamaha wa jumla.”

Mwisho, Muungano wa Wanazuoni wa Kiislamu ulilaani hatua ya walowezi ya kuvamia eneo la Msikiti wa Al-Aqsa na kutekeleza ibada za Kitalmudi chini ya jina la “Baraka za Makuhani na Kusujudu Kishujaa”, huku kukiwa na ukimya unaolaumiwa kutoka upande wa Waarabu na Waislamu. Ulisisitiza: Mashambulizi haya yanathibitisha kwamba hakuna suluhisho lolote pamoja na utawala wa Kizayuni isipokuwa Muqawama; ambao ndiyo njia pekee ya kurejesha ardhi, heshima na utu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha